Genesis 15:1-6

Agano La Mungu Na Abramu

1 aBaada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu.
Mimi ni ngao yako,
na thawabu yako kubwa sana.”

2 bLakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?” 3 cAbramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”

4 dNdipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.” 5 eAkamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”

6 fAbramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.

Copyright information for SwhKC